Hakuna furaha ya kudumu itakayotengenezwa na mtu kwa kuwakosesha wengine amani. -Unaweza kufanikiwa bila kufelisha wengine. -Unaweza kuinuka bila kushusha wengine. -Unaweza kubarikiwa bila kulaani wengi e. Mungu ni pendo na kwasababu tuliumbwa kwa mfano wake na sisi ni wake tunakumbushwa kuwa hapa duniani si kwetu kwasababu tunayo makazi ya kudumu ambayo ni alipo baba yetu Mungu. Hakuna haja wala faida ya kuchukiana. Wacha pendo lake Kristo litawale AMEN .